Barua ya Mwezi Novemba 2001
UNAWEZA
KUJIFUNZA KUOMBA KWA MAFANIKIO ZAIDI KULIKO UOMBAVYO SASA
Mpendwa
katika Kristo Yesu,
Tulipokuwa tukitafakari
katika Roho juu ya yale ambayo Mungu anataka tukuandikie mwezi huu
tuliona ndani yetu tunasukumwa kukutia moyo kwa kusema ya kuwa, “
Unaweza kujifunza kuomba kwa mafanikio zaidi kuliko uombavyo sasa”
Tunaamini neema ya Mungu iko
juu yako ili kukusaidia uzidi kuwa na kiu ya kufanikiwa katika maeneo na
mambo yote katika Bwana. Ni lengo zuri na lenye nia nzuri ya kuona
Kristo akijitukuza katika maisha yako.
Kuna siku wanafunzi waliwahi
kumwambia Bwana Yesu maneno haya: “Bwana, tufundishe sisi kusali,
kama vile Yohana alivyowafundisha wanafunzi wake”. Hii inaonyesha
jinsi ambavyo walitamani wawe na mafanikio mazuri katika maombi yao ya
kila siku.
Kuna
aina mbali mbali za maombi
Kama vile kulivyo na aina
mbalimbali za michezo ya mpira na taratibu za kucheza zinazotofautiana,
na maombi ni vivyo hivyo. Kuna aina mbalimbali za maombi na taratibu
zake za kuomba zinatofautiana.
Kama vile ambavyo huwezi
kutumia taratibu za kucheza mpira wa miguu katika kutaka zikusaidie
ushinde unapocheza mpira wa vikapu, vivyo hivyo na maombi. Taratibu za
kuomba maombi ya aina fulani zinaweza zikakufanya ushindwe kujibiwa
maombi yako utakapozitumia katika maombi ya aina nyingine.
Waefeso 6:18 inasema, “
Kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho mkikesha kwa
jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote”
“Kwa sala zote”
wakati mwingine ina maana ya “Kwa aina mbalimbali za maombi”.
Kwa sababu neno “zote” linatumika kuonyesha ya kuwa kuna aina
za sala au maombi zaidi ya moja. Na Mtume Paulo anataka
tusali kwa sala zote. Huwezi kuomba sala zote kama huzijui zote! Unaweza
ukajikuta unatumia aina moja tu ya sala au maombi katika kuombea shida
zote ulizonazo, na unabaki unajiuliza kwa nini maombi mengine umejibiwa
na mengine hujajibiwa.
Kwa mfano, angalia aina
zifuatazo za maombi na uzijue zinavyotofautiana:
- Maombi
ya kupokea wakati huo huo unapoomba (Marko 11:24)
- Maombi
yanayojua mapenzi ya Mungu juu ya jambo unaloliombea (1Yohana
5:14,15)
- Maombi
unayoomba jambo ambalo huna uhakika kama ni mapenzi ya Mungu kwako
au kwa yule unayemuombea. (Mathayo 26:36 – 42, Warumi 8:26, 27)
4.
Kuomba maombi bila
kuacha kuomba hadi au mpaka umepata unachoomba. (Luka 18:1 –8, Luka
11:9 – 13, Isaya 62:6,7)
- Kuomba
maombi ya kudai upewe haki yako. (Isaya 43:26)
Hii
ni mifano michache tu ya maombi na matumizi yake na taratibu zake za
kuomba vinatofautiana. Tunachoomba kwa Mungu kwa ajili yako unaposoma
barua hii, ni ya kuwa “Bwana azidi kukufundisha kuomba kwa
mafanikio kuliko uombavyo sasa”. Tunaamini Roho Mtakatifu yuko
pamoja nawe katika kujifunza huku.
Tunahitaji
maombi yako
Tarehe 5 – 9 Disemba 2001
tutakuwa na semina ya Neno la Mungu Iringa Mjini itayojumuisha watu wa
madhehebu mbalimbali. Tunahitaji maombi yako ili Mungu atumiminie upako
wa mafuta ya Roho Mtakatifu katika kufanikisha maandalizi ya semina; na
katika kufanikisha semina yenyewe katika kila eneo.
Jina la Bwana na litukuzwe tunapozidi kukumbukana katika maombi.
Ni
sisi watumishi wa Kristo,
Christopher
na Diana Mwakasege