Yesu Akamwambia "Lisha Kondoo Zangu" (Yohana 21:17)
Home
Maombi
Ratiba
Shuhuda
Mafundisho
Maswali na Majibu
Barua za Mwezi
Kuchangia Huduma

Barua ya Mwezi Oktoba 2004                                                            Kutoka kwa Christopher na Diana Mwakasege


INAWEZEKANA MUNGU AMEJIBU ILA JIBU
HALIJAJIDHIHIRISHA
BADO KWA SABABU YA UPINZANI.

Salamu katika Jina la Yesu;

Kwa wale wanaosoma biblia wanakumbuka habari za nabii Danieli alivyoomba kwa kufunga kwa muda wa siku ishirini na moja "bila kupata jibu lo lote la Mungu"

Nabii Danieli anatuambia hivi: " Katika siku zile mimi, Danieli, nalikuwa nikiomboleza muda wa majuma matatu kamili. Sikula chakula kitamu, wala nyama wala divai haikuingia kinywani mwangu, wala sikujipaka mafuta kabisa, hata majuma matatu kamili yalipotimia" (Danieli 10:2,3).

Siku ya ishirini na nne  malaika Gabrieli alimtokea na kumwambia maneno haya: "Usiogope, Danieli; kwa maana tangu siku ile ya kwanza ulipotia moyo wako ufahamu, na kujinyenyekeza mbele za Mungu wako, maneno yako yalisikiwa; nami nimekuja kwa ajili ya maneno yako. Lakini mkuu wa ufalme wa Uajemi alinipinga siku ishirini na moja; bali, tazama, huyo Mikaeli, mmoja wa hao wakuu wa mbele, akaja kunisaidia ..." (Danieli 10:12,13)

Nabii Danieli alikaa kwenye maombi siku ishirini na moja, huku akidhani Mungu hajajibu maombi yake. Lakini malaika Gabrieli alipomtokea katika siku ya ishirini na nne alimwarnbia wazi ya kuwa maombi yake yalisikiwa na kujibiwa siku ile ile ya kwanza aliyoanza kuomba.

Malaika Gabrieli alimweleza Danieli jinsi ambavyo kutokana na kujibiwa rnaombi yake siku ile ile ya kwanza, alitumwa aje amIetee majibu.

Ukifuatilia utaona ya kuwa kati ya Danieli kuomba na Mungu kujibu rnaombi yake hakuna tofauti ya siku wala kuchelewa. Maana Mungu alijibu maombi ya Danieli siku ile ile ambayo Danieli aliomba!

Ila kati ya maombi ya Danieli kujibiwa na majibu ya maombi kudhihirika  kwa Danieli kulikuwa na tofauti ya siku ishirini na nne!

Danieli angejua toka siku ya kwanza ya kuwa maombi yake yamejibiwa asingeendelea kuomba, bali angeendelea kumshukuru Mungu hadi majibu ya maombi yake yamedhihirika kwake.

Hii huwa inatokea mara kwa mara kwa watu wa Mungu wengi,ingawa wanakuwa ni wagumu kulikubali.  Mungu huwa anajibu rnaombi yao, na moyoni wanashuhudiwa Mungu amejibu lakini hawaamini! Kwa nini? Kwa sababu hawajaona jibu limejidhihirisha!

Lakini tunataka tukutie moyo ya kuwa ikiwa umeomba jambo kwa Mungu, na moyoni unashuhudiwa ya kuwa Mungu amekujibu ingawa 'kwa nje' bado jibu lenyewe hujaliona -usikae mkao wa kutokuamini!

Wewe endelea kumshukuru Mungu kwa majibu yake, na ikibidi endelea kumkemea shetani na kumpinga sawasawa na Yakobo 4:7. Baada ya muda jibu lako litajidhihirisha.

Inawezekana Mungu amejibu maombi
yako lakini wewe hujui – na unadhani

Mungu amechelewa kukujibu!

Kuna mifano kadhaa katika biblia ambayo Yesu alijibu maombi ya watu na wale watu wakapokea majibu yao bila kwanza kuona  majibu hayo kwa jinsi ya nje!

Mfano mmojawapo ni wa yule mama wa kiyunani katika kabila ya Kisoforoinike. Alikwenda kwa Yesu kuomba amponye binti yake ambaye alikuwa amepagawa na pepo. Yule mama hakuwa amemchukua mtoto wake mgonjwa alipokwenda kwa Yesu - alikwenda peke yake.

Yesu alimwambia; "… enenda zako; pepo amemtoka binti yako" (Mathayo 9:29). Binti mgonjwa hakuwa karibu nao Yesu alipotamka maneno hayo, na kwa hiyo isingekuwa rahisi kwa yule mama kuyapokea maneno hayo ya Bwana Yesu kama majibu ya maombi yake.

Lakini tunaona ya kuwa yule mama, "akaenda zake nyumbani kwake, akamkuta yule kijana amelazwa kitandani, na yule pepo amekwisha kumtoka" (Mathayo 9:29).

Huyu mama alifanya kitendo cha kwenda nyumbani akiamini ombi lake lake limejibiwa ingawa kwa macho halikuwa hajaliona hilo jibu hadi alipofika nyumbani. Asingeyaamini maneno ya Bwana Yesu asingeondoka bali angabaki na kuendelea kuomba. Au angetakata tamaa na kuogopa kurudi nyumbani kwa mtoto wake. Lakini tunaona yule mama akifanya kitendo cha kwenda nyumbani akionyesha kuwa aliyaamini maneno ya Yesu aliyosema juu ya mtoto wake mgonjwa hata kabla hajayaona matokeo yaa maneno hayo kwa macho.

Ndiyo maana tunakwambia ya kuwa inawezekana Mungu amejibu maombi yako, lakini wewe hujui, na unadhani Mungu amechelewa kukujibu. Je, umechukua hatua ya kufuatilia eneo lile ulilotegemea jibu litokee ili ukaone kama limetokea au la? Chukua hatua ya imani kama ya yule mama, nenda kamwangalie 'mtoto', utamkuta amepona kama vile Yesu alivyosema.

Kumbuka Yesu alipomjibu yule mama, hakumpa yule mama jibu la ombi lake ili ampelekee mtoto wake, bali Yesu aliamua kulituma jibu la ombi la mama yule kwa mtoto  wake ambalo ndipo mahali lilipotakiwa kwenda. Yesu akamwambia yule mama  alichofanya, na kamwambia aende zake maana jibu la ombi lake limetumwa lilikotakiwa.

Mfano mwingine tunauona pale ambapo Yesu alimponya mtumwa wa akida  mmoja kama tunavyosoma habari hii katika kitabu cha Luka 7:2 –10.

Kama ilivyokuwa kwa mama wa Kiyunani ndivyo ilivyokuwa kwa akida huyu. Jibu lake lilitumwa moja kwa moja kwa mgonjwa naye akapona wakati akiwa mbali na yule akida na wazee wa Kiyahudi waliomwombea kwa Yesu.

Yule akida ndicho alichoomba! Maana alisema "…sema neno tu, na mtumwa wangu atapona" (Luka 7:7). Yesu aliishangaa sana imani hiyo,.kwa sababu si wengi wanayo imani ya jinsi hiyo, kwa kuwa wengi wanataka kuona jibu la maombi yao kabla hawajaamini ya kuwa wamejibiwa! ‘Neno’ kwa wengi halitoshi kuwa jibu la maombi yao!

Mfano mwingine ni wakati Yesu alipomponya mtoto wa diwani mmoja bila mtoto huyo kuwa karibu na mahali maombi yalipokuwa yanafanyikia.

Hali ya mtoto wa diwani ilikuwa mbaya karibu na kufa, na akamwomba Yesu aende nyumbani kwake amponye.

Badala ya Yesu kwenda nyumbani kwa diwani, akamwambia diwani; "enenda,Mwanao yu hai" (Yohana 4:50)

Yule diwani angeweza kusita na kutokuamini na kuendelea kuomba au kuacha kuomba kwa kukata tamaa. Lakini badala yake tunaona ya kuwa, "akalisadiki lile neno aliloambiwa na Yesu, naye akashika njia" (Yohana 4:50). Na alipofika nyumbani alimkuta mtoto wake mzima.

Cha ajabu ni kwamba alipomkuta amepona aliwauliza wale waliokuwa wanamtunza mtoto wake mgonjwa saa ambayo mtoto wake alipona!  “ …. Wakamwambia, jana, saa saba, homa ilimwacha. Basi babaye akafahamu ya kuwa ni saa ile ile aliyoambiwa na Yesu, Mwanao yu hai” (Yohana 4:52,53).

Katika mfano wa huyu diwani tunaona jinsi ambavyo tofauti kati ya yeye kujibiwa maombi yake na yeye kuyaona majibu ya maombi yake ni siku moja nzima. Maana alipofika nyumbani na kumkuta mtoto wake amepona na kuuliza saa aliyopona, aliambiwa ni “jana, saa saba, homa ilimwacha”.

Je, maombi yako yamejibiwa “jana” lakini hujui? Je! Umeulizia au umefuatilia huko ulikotaka majibu ya maombi yako yadhihirike ili uone kama yamefika au la?.
          Unaweza ukawa unalalamika na kunung’unika kwamba Mungu amechelewa kujibu maombi yako, na kumbe yalikwishajibiwa ‘jana’ na wewe hujui!

Tuzidi kuombeana!

UNATAKA KUOKOKA?
Kama unataka kumpa YESU maisha yako sasa, bonyeza hapa
©2003 Tanzania Social and Economic Trust.  All Rights Reserved.