Yesu Akamwambia "Lisha Kondoo Zangu" (Yohana 21:17)
Home
Maombi
Ratiba
Shuhuda
Mafundisho
Maswali na Majibu
Barua za Mwezi
Kuchangia Huduma
JIHADHARI NA MAFUNUO


Utangulizi

JIHADHARI NA MAFUNUO

    Nafahamu ya kuwa mara tu baada ya kusoma kichwa cha somo hili, ulianza kujiuliza maswali mbali mbali juu ya mafunuo.     
                Jihadhari na Mafunuo! Huu ni ujumbe muhimu uliomo katika somo hili. Si mafunuo yote ni ya Mungu au yanatoka kwa Mungu. Mafunuo maana yake nini? Chanzo cha kuwepo mafunuo ni nini! Utayafahamu kwa njia gani au kwa namna gani mafunuo yasiyokuwa ya Mungu?          
                Haya ni baadhi tu ya maswali mengi yanayojibiwa katika somo hili. Naamini kabisa ya kuwa Roho Mtakatifu aliyekuongoza kulisoma somo hili hivi sasa, atakuwa pamoja nawe katika kukuelewesha kwa undani na ufasaha zaidi mambo niliyoyaandika.    
                Kumbuka hizi ni siku za mwisho na kurudi kwa Bwana Yesu Kristo mara ya pili kuja kulichukua kanisa kumekaribia sana. Bwana na atuwezeshe katika kutafakari  maneno yaliyomo katika somo hili, ili siku ajapo tusiwe watu wa kuaibika mbele zake – bali tuwe watu wa kufurahi na kumsifu milele na milele – Amina! Kila wiki kwa wiki sita mfululizo tutakuwa tunajifunza sehemu ya somo hili. Ni matumaini yangu utakuwa pamoja nami kila wiki!  


Wiki ya Kwanza: MAFUNUO
Wiki ya Pili:
Mambo matano muhimu unayohitaji kujua juu ya Mafunuo
Wiki ya Tatu: Kwa nini tupime mambo yote?
Wiki ya Nne: Tutapima mambo yote kwa namna gani?
Wiki ya Tano: Hila za ibilisi ndani ya Kanisa
Wiki ya Sita: Tatizo la Wakristo na dawa yake

Jihadhari na Mafunuo / utang / 1 / 2 / 3 / 4 / 5 / 6 /

UNATAKA KUOKOKA?
Kama unataka kumpa YESU maisha yako sasa, bonyeza hapa
©2003 Tanzania Social and Economic Trust.  All Rights Reserved.