Utangulizi
JIHADHARI
NA MAFUNUO
Nafahamu ya kuwa mara tu baada ya kusoma kichwa cha somo hili, ulianza
kujiuliza maswali mbali mbali juu ya mafunuo.
Jihadhari na Mafunuo! Huu ni ujumbe muhimu uliomo katika somo hili. Si
mafunuo yote ni ya Mungu au yanatoka kwa Mungu. Mafunuo maana yake nini?
Chanzo cha kuwepo mafunuo ni nini! Utayafahamu kwa njia gani au kwa
namna gani mafunuo yasiyokuwa ya Mungu?
Haya ni baadhi tu ya maswali mengi yanayojibiwa katika somo hili.
Naamini kabisa ya kuwa Roho Mtakatifu aliyekuongoza kulisoma somo hili
hivi sasa, atakuwa pamoja nawe katika kukuelewesha kwa undani na ufasaha
zaidi mambo niliyoyaandika.
Kumbuka hizi ni siku za mwisho na kurudi kwa Bwana Yesu Kristo mara ya
pili kuja kulichukua kanisa kumekaribia sana. Bwana na atuwezeshe katika
kutafakari maneno yaliyomo
katika somo hili, ili siku ajapo tusiwe watu wa kuaibika mbele zake –
bali tuwe watu wa kufurahi na kumsifu milele na milele – Amina! Kila
wiki kwa wiki sita mfululizo tutakuwa tunajifunza sehemu ya somo hili.
Ni matumaini yangu utakuwa pamoja nami kila wiki!
Wiki ya Kwanza: MAFUNUO
Wiki ya Pili: Mambo
matano muhimu unayohitaji kujua juu ya Mafunuo
Wiki ya Tatu: Kwa
nini tupime mambo yote?
Wiki ya Nne: Tutapima
mambo yote kwa namna gani?
Wiki ya Tano: Hila
za ibilisi ndani ya Kanisa
Wiki ya Sita: Tatizo
la Wakristo na dawa yake
Jihadhari
na Mafunuo / utang / 1 / 2
/ 3 / 4 / 5
/ 6 /