Sura ya Saba
UKITOA
TEGEMEA KUPOKEA
Sehemu nyingi nilizotembelea
nimeona na kufahamu ya kuwa watu wengi wanatoa sadaka – fedha
taslimu au vitu au wanyama kwa Mungu BILA KUTEGEMEA KUPOKEA KUTOKA KWA
MUNGU.
Furaha ya utoaji inatokana na kufahamu matokeo ya utoaji huu.
Ndiyo maana mkristo yuko tayari kuweka shilingi 10,000/= katika mradi
utakaompa faida kuliko kutoa kanisani ambako anafikiri sadaka hiyo
haina faida kwake binafsi. Kwa hiyo siku zote atatoa sadaka kidogo
kanisani au kwenye kazi ya Mungu.
Bila ya mkristo kujua kwamba anajua na kuwa na uhakika moyoni mwake
kuwa akitoa sadaka anastahili kupokea ZAIDI YA KIWANGO ALICHOTOA
KUTOKA KWA MUNGU –
utoaji wake utakuwa chini siku zote.
Wakristo wengi wanafikiri
wakimtolea Mungu kitu, watazidi kupungukiwa na kufilisikia. Lakini
ukweli wa mambo ni kwamba ukimtolea Mungu ulicho nacho UNAFUNGUA
MLANGO WA KUFANIKIWA kwa ulivyo navyo. Unapomtolea Mungu hufilisiki
bali unatajirika!
Tunapokuwa
ndani ya Kristo, tunachukua na kubeba tabia ya Mungu ndani yetu.
Imeandikwa hivi:
“ Bali wote
waliompokea(Kristo) aliwapa UWEZO wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio
wale waliaminio jina lake” (Yohana 1:12) “ Kwa kuwa UWEZA wake wa
UUNGU umetukirimia vitu vyote vipasavyo uzima na utauwa, kwa kumjua
yeye aliyetuita kwa utukufu wake na wema wake mwenyewe”
(1Petro 1:13)
Ni vizuri ufahamu ya kuwa
mojawapo ya tabia ya Uungu tuliyo nayo ndani yetu katika Kristo ni
tabia ya kutoa HUKU UKITEGEMEA KUPOKEA. Mungu akitoa kitu anategemea
kupokea.
Tabia
ya Mungu ya Utoaji
Mungu alipokuwa anamtoa mwana wake wa pekee,
alimtoa huku akitegemea kupata watoto wengi wa kiroho. “Kwa maana
jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanae pekee, ili
kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele” (Yohana
3:16)
Mungu
alipokuwa anamtuma Roho Mtakatifu juu ya wanafunzi wake, alimtoa huku
akitegemea kupata mashahidi wengi watakaosimama upande wake na
kulitetea jina lake hapa duniani. “Lakini mtapokea nguvu, akiisha
kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu
katika Yerusalem, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho
wa nchi” (Matendo ya Mtume 1:8)
Mungu
anapotoa utajiri kwa watu wake, anautoa huku akitegemea kupata agano
lililo imara kati yake na wanadamu. “ Bali utamkumbuka Bwana, Mungu
wako, maana ndiye akupaye nguvu za kupata utajiri; ili alifanye imara
agano lake alilowapa baba zako,kama hivi leo”
(Kumbukumbu la Torati 8:18).
Hii ndiyo tabia tuliyo nayo ndani ya Kristo, kutoa huku tukitegemea
kupokea. Hili jambo la kutoa na kupokea wakati mwingine linajulikana
kama KUPANDA na KUVUNA.
Hakuna mkulima anayepanda mbegu shambani bila kutegemea kuvuna. Kama
hana tegemeo la kuvuna, basi hata haja na hamu ya kupanda inapotea –
inakuwa haina maana kupanda maana hatapata kitu.
Katika mambo ya kiroho ni vivyo hivyo. Utakachotoa ndicho utakachopata.
Utakachopanda ndicho utakachovuna. Ukipanda fedha utavuna fedha.
Ukipanda upendo utavuna upendo. Ukipanda ng’ombe utavuna ng’ombe.
Ukitoa vitabu utapokea vitabu. Imeandikwa hivi; “
Msidanganyike, Mungu hadhihakiwi; kwa kuwa cho chote apandacho mtu,
ndicho atakachovuna” (Wagalatia 6:7).
Hivi ndivyo ilivyo, utakachopanda ndicho utakachovuna. Kwa maneno
mengine, ni kwamba ukipanda tegemea kuvuna.
Tumia
tabia ya Mungu iliyo ndani yako
Ikiwa wewe unakaa ndani ya Kristo
na Kristo anakaa ndani yako, basi uwe na uhakika ya kuwa tabia ya
Uungu ya kutoa na kupokea, kupanda na kuvuna imo ndani yako.
Inaonekana wazi ya kuwa wakristo wa kanisa la Korintho na Filipi
katika nyakati za huduma ya Mtume Paulo – walishiriki sana katika
habari hii ya kutoa na kupokea. Siyo kutoa bila kupokea bali kutoa na
kupokea. Hii ni tabia iliyoonekana wazi katika ukristo wao. Hebu soma
maneno yafuatayo juu ya habari hii katika kitabu cha Wafilipi
katika nyakati za huduma ya Mtume Paulo – walishiriki sana katika
habari hii ya kutoa na kupokea. Siyo kutoa bila kupokea bali kutoa na
kupokea. Hii ni tabia iliyoonekana wazi katika ukristo wao. Hebu soma
maneno yafuatayo juu ya habari hii katika kitabu cha Wafilipi 4:10-14;
“
Nalifurahi sana katika Bwana, kwa kuwa sasa
mwisho mmehuisha tena fikra zenu kwa ajili yangu, kama
vile mlivyokuwa mkinifikiri hali yangu; lakini mkupata nafasi. Si
kwamba nasema haya kwa kuwa
nina mahitaji; maana nimejifunza kuwa radhi na hali
yo yote niliyo nayo.
Najua kudhiliwa, tena najua kufanikiwa; katika hali yo yote, na katika
mambo yo yote, nimefudishwa kushiba na kuona njaa, kuwa na vingi na
kupungukiwa. Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu. LAKINI
MLIFANYA VEMA, mliposhiriki nami katika dhiki yangu”.
Mtume
Paulo hapa anawaambia Wafilipi wazi kuwa maisha yake yote na katika
mambo yote na katika hali yo yote tumaini lake na ushindi wake ni
katika UWEZA WA KRISTO amtiaye nguvu – na wala si katika uweza wake
Paulo au huruma za wanadamu. Hata hivyo aliwaambia “MLIFANYA VEMA
MLIPOSHIRIKI NAMI KATIKA DHIKI YANGU”. Katika maneno yanayofuata
aneleza kwa nini walifanya vema kumhudumia katika dhiki yake.
“Nanyi pia, ninyi wenyewe mnajua, enyi Wafilipi, ya kuwa katika
mwanzo wa Injili, nilipotoka Makedonia, hakuna kanisa
lingine lililoshirikiana nami katika habari hii ya
KUTOA NA
KUPOKEA, ila ninyi peke yenu. Kwa kuwa hata
huko Thesalonike mliniletea msaada kwa mahitaji yangu,
wala si mara moja. Si kwamba nakitamani kile kipawa, bali NAYATAMANI
MAZAO YANAYOZIDI KUWA MENGI, katika HESABU YENU”
(Wafilipi 4:15 – 17).
Ni
wazi kabisa ya kuwa kwa sababu ya kushiriki katika habari ya KUTOA NA
KUPOKEA – Wafilipi hawakufilisika wala kupungukiwa bali MAZAO
YALIZIDI KUWA MENGI KATIKA HESABU YAO. Huyu Mungu aliyewafanikisha
Wafilipi, ndiye atakayekufanikisha wewe na kuongeza mazao mengi katika
habari hii ya KUTOA na KUPOKEA.
Kumbuka
siku zote kuishi kwa kuitumia na kutegemea tabia ya Mungu iliyo ndani
yako katika Kristo. Tabia hii itakusaidia kutoa na kutegemea kupokea
– kupanda na kutegemea kuvuna. Imeandikwa hivi
“Wapeni
watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwa
– sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu”
(Luka 6:38)