Yesu Akamwambia "Lisha Kondoo Zangu" (Yohana 21:17)
Home
Maombi
Ratiba
Shuhuda
Mafundisho
Maswali na Majibu
Barua za Mwezi
Kuchangia Huduma
NAMNA YA KUSHIRIKI KUOMBEA WENGINE

Ndugu katika Kristo,

Naamini kuwa umefungua ukurasa huu kwa sababu una huduma ya maombezi na una mzigo wa kuombea wengine wenye shida na mahitaji mbalimbali.

Tunakukaribisha ujiunge na Mailing List ya maombezi itakayokuwezesha kupata, kwa njia ya email, mahitaji na shida mbalimbali zinazohitaji huduma yako ya maombezi. Mailing List ni mtandao wa mawasiliano kupitia barua pepe yaani email.
Kujiunga ni rahisi sana. Inahitajika email address yako tu. Namna ya kujiunga:
1. Tuma email kwa "maombi-request@kicheko.com"
2. Usiandike chochote katika  sehemu ya "Subject"
3. Sehemu ya ujumbe andika "subscribe"
4. Halafu itume.
Komputa itasoma na kutambua email address yako, itakuunganisha na kukupa majibu papo hapo.

Kama unataka kumuunganisha rafiki yako katika hatua ya 3 baada ya neno "subscribe" andika email address ya rafiki yako. Kwa mfano kama email address yake ni rafiki@kicheko.com basi katika hatua ya tatu hapo juu utaandika "subscribe   rafiki@kicheko.com. Komputa itamtumia ujumbe wa kumtaka athibitishe.

Kwa kujiunga na mtandao huu utapata emails zenye mahitaji ya maombezi na unachotakiwa kufanya ni kuwaombea ndugu hao sawasawa na mahitaji yao. Mungu akubariki sana.
UNATAKA KUOKOKA?
Kama unataka kumpa YESU maisha yako sasa, bonyeza hapa
©2003 Tanzania Social and Economic Trust.  All Rights Reserved.